Breaking News:

Top Ad

//

Kambi ya Maalim Seif yatangaza mkakati wa kujibu ‘timuatimua’ ya Lipumba





Siku chache baada ya Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) anayetambulika na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba kutangaza kuwafukuza wabunge nane wa viti maalum na madiwani, Kambi ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif imejibu.
Akizungumza na waandishi wa habari, Naibu Katibu wa CUF (Zanzibar), Nassor Ahmed Mazrui amesema kuwa wanajipanga kufanya kikao vikao vya Kamati ya Utendaji na Baraza Kuu la chama hicho kujadili uamuzi uliotangazwa na Profesa Lipumba huku akidai kuwa ni uamuzi batili uliotokana na Baraza batili.
“Baraza Kuu halali la chama litatoa uamuzi wa nini muelekeo wa uamuzi uliotolewa na hawa watu ambao wengine tuliwasimamisha uanachama,” alisema Mazrui.
Julai 23 mwaka huu, Profesa Lipumba alitangaza uamuzi wa Baraza Kuu la chama hicho la kuwaondoa wabunge nane wa viti maalum kwa madai ya usaliti, hujuma na utovu wa nidhamu dhidi ya Mwenyekiti (yeye) na Naibu Katibu Mkuu (Bara), Magdalena Sakaya.

Post a Comment

0 Comments